1. |
Naapa kwa tini na zaituni! |
2. |
Na kwa Mlima wa Sinai! |
3. |
Na kwa mji huu wenye amani! |
4. |
Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa. |
5. |
Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini! |
6. |
Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha. |
7. |
Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo? |
8. |
Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote? |