95. At-Tin

1.

Naapa kwa tini na zaituni!

2.

Na kwa Mlima wa Sinai!

3.

Na kwa mji huu wenye amani!

4.

Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.

5.

Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!

6.

Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.

7.

Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?

8.

Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?