94. Ash-Sharh’

1.

Hatukukunjulia kifua chako?

2.

Na tukakuondolea mzigo wako,

3.

Ulio vunja mgongo wako?

4.

Na tukakunyanyulia utajo wako?

5.

Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,

6.

Hakika pamoja na uzito upo wepesi.

7.

Na ukipata faragha, fanya juhudi.

8.

Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.