1. |
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama! |
2. |
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu! |
3. |
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake? |
4. |
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake! |
5. |
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake. |
6. |
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama? |
7. |
Basi jicho litapo dawaa, |
8. |
Na mwezi utapo patwa, |
9. |
Na likakusanywa jua na mwezi, |
10. |
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio? |
11. |
La! Hapana pa kukimbilia! |
12. |
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu. |
13. |
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha. |
14. |
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake. |
15. |
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru. |
16. |
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka. |
17. |
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha. |
18. |
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake. |
19. |
Kisha ni juu yetu kuubainisha. |
20. |
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani, |
21. |
Na mnaacha maisha ya Akhera. |
22. |
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng’ara, |
23. |
Zinamwangallia Mola wao Mlezi. |
24. |
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana. |
25. |
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo. |
26. |
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo, |
27. |
Na pakasemwa: Nani wa kumganga? |
28. |
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki; |
29. |
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi, |
30. |
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi! |
31. |
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali. |
32. |
Bali alikanusha, na akageuka. |
33. |
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao. |
34. |
Ole wako, ole wako! |
35. |
Kisha Ole wako, ole wako! |
36. |
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure? |
37. |
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa? |
38. |
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo. |
39. |
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke. |
40. |
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu? |