114. An-Nas

1.

Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu,

2.

Mfalme wa wanaadamu,

3.

Mungu wa wanaadamu,

4.

Na shari ya wasiwasi wa Shetani, Khannas,

5.

Anaye tia wasiwasi katika vifua vya watu,

6.

Kutokana na majini na wanaadamu.