113. Al-Falaq

1.

Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,

2.

Na shari ya alivyo viumba,

3.

Na shari ya giza la usiku liingiapo,

4.

Na shari ya wanao pulizia mafundoni,

5.

Na shari ya hasidi anapo husudu.