110. An-Nas’r

1.

Itakapo kuja nusura ya Mwenyezi Mungu na ushindi,

2.

Na ukaona watu wanaingia katika Dini ya Mwenyezi Mungu kwa makundi,

3.

Zitakase sifa za Mola wako Mlezi, na umwombe msamaha; hakika Yeye ndiye anaye pokea toba.