107. Al-Maau’n

1.

Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo?

2.

Huyo ndiye anaye msukuma yatima,

3.

Wala hahimizi kumlisha masikini.

4.

Basi, ole wao wanao sali,

5.

Ambao wanapuuza Sala zao;

6.

Ambao wanajionyesha,

7.

Nao huku wanazuia msaada.