106. Quraish

1.

Kwa walivyo zoea Maqureshi,

2.

Kuzoea kwao safari za siku za baridi na siku za joto.

3.

Basi nawamuabudu Mola Mlezi wa Nyumba hii,

4.

Ambaye anawalisha wasipate njaa, na anawalinda na khofu.