1. |
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo? |
2. |
Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? |
3. |
Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi, |
4. |
Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni, |
5. |
Akawafanya kama majani yaliyo liwa! |