1. |
Inayo gonga! |
2. |
Nini Inayo gonga? |
3. |
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga? |
4. |
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika; |
5. |
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa! |
6. |
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, |
7. |
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza. |
8. |
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, |
9. |
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya! |
10. |
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo? |
11. |
Ni Moto mkali! |